Wafungwa 7 wafariki na wengine 9 wajeruhiwa katika ghasia zilizotokea katika gereza moja nchini Mexico.
Ghasia zilizotokea katika gereza moja nchini Mexico zimepelekea wafungwa 7 kufariki na wengine 9 wamejeruhiwa vikali.
GHasia hizo zimetokea katika gereza lenye ulinzi mkali katika jimbo la Puente Grande.
Kulingana na taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari nchini Mexico, wafungwa walishambulia kwa silaha za moto na visu na kusababisha vifo hivyo na majeruhi.
Hali imerejea kuwa shwari baada ya maafisa magaereza kuingilia kati.
Uchunguzi umeanzishwa kubaini sababu na ghasia hizo.